Upishi wa tembele la chukuchuku
Mahitaji Matembele mafungu 2 Nyanya 2 kubwa Kitunguu 1 Chumvi kiasi Mafuta kijiko 1 Ndimu 1 Namna ya kutengeneza Chukua matembele , yachambue na kisha yaoshe. Weka kwenye sufuria ya kupikia. Kata kata nyanya, kitunguu na weka juu yake. Kisha weka chumvi na mafuta na injika jikoni. Weka moto wa kiasi na acha viive kwa muda wa dakika tano. Funua na geuza, vitu vyote vitakuwa vimeiva. Kamulia ndimu na kisha ipua. Matembele yako yatakuwa tayari kwa kuliwa. Waweza kula na ugali ama chakula kingine utakachopendelea.