Posts

Doughnuts

Image
Mahitaji Siagi                             1/2 kg Sukari   (iliyosagwa)    1/2 kg Mayai                           6 Unga                            1kg Baking powder            2 teaspoons Kungu manga               1 Namna ya kupika Changanya unga pamoja na kungu manga na baking powder na siagi , Tia yai moja moja hadi uwe donge Kata vidonge vidonge na usukume kama chapatti, kisha kata duara na chukua kifuniko kata katikati ya mduara. Chemsha mafuta jikoni na kisha uchome kiasi kiasi hadi ziishe zote. Vikipata rangi ya udhurungi ipua na nyunyizia sukari, tayari kwa kuliwa  

Nyama ya kukunja

Image
Mahitaji Nyama                         ½ kg Mayai               5 (manne yachemshe) Ndimu              2 Chumvi            kiasi kitunguu saumu             punje tatu Pilipili              kiasi (menya kata) Namna ya kupika Changanya nyama na tangawizi na thomu na pilipili Weka karatasi juu ya kibao, tandaza nyama na panga mayai juu yake Kunja karatasi na wacha nafasi pembeni na funga uzi Injika chuma tia samli na kaanga halafu yake geuza kila upande kwa upesi Ipua na weka ipowe na kula, kata kwa kiasi
Image
Mahitaji Unga wa ngano wa Atta nusu kilo Mtindi robo lita Maji ya vuguvugu kiasi cha kukandia Hamira kijiko kimoja cha chai Chumvi kiasi kama utapendelea Trei za kuokea mikate Namna ya kuandaa Chukua bakula kavu na kubwa kiasi   la kukandia unga wako. Weka unga, chumvi na kisha hamira. Changanya mchanganyiko wako huo kabla ya kutia majimaji . kisha weka maziwa ya mtindi endelea kuchanganya hadi ukandike. Kama una maziwa ya mtindi ya kutosha, unaweza kukanda kwa kutumia maziwa hayo pekee hadei unga wako ulainike kabisa. Wakati ukiendelea kukanda kama utaona kuna haja ya kuongeza maji waweza ongeza yale ya uvuguvugu. Ukishalainika acha uumuke inaweza kuwa kwa muda wa dakika 20 hadi 30, hii itategemea na ukali wa hamira uliyotumia. Ukishaumuka, chukua na ukande tena baada ya hapo kata na weka kwenye trei za kuokea mkate. Funika na acha kwa muda wa dakika tano hadi sita . Kisha anza kuoka kwa moto wa kiasi. Hakikisha unaiva na kuwa wa