Wali wa kuaanga




Mahitaji
Kiporo cha wali wa Jasmine vikombe viwili vya chai
Majani ya kitunguu maji  matatu hadi manne yaliyokatwa katwa
Punje 3 -4 za kitunguu saumu kilichopondwa
Sosi ya soya vijiko viwili vya chai
Sosi ya samaki nusu kijiko cha chai
Nyama ya samaki aina ya kaa
Yai moja
Sukari nusu kijiko
Mafuta ya alizeti kiasi
Vya kupambia
Kipande kimoja cha ndimu
Tango silesi mbili au tatu
Sosi ya samaki, Pilipili ndefu na limao
Namna ya kupika
Chukua chuma cha kukaangia chapatti na weka mafuta kiasi na kisha weka vitunguu saumu na kanga hadi viwe vya hudhurungi. Kisha weka yai na endelea kukaanga hadi liive.  Weka nyama ya kaa na endelea kukaanga. Baada ya hapo miminia  wali na endelea kukaanga huku ukiuchanganya vizuri. Miminia sosi ya soya na halafu ya samaki kabla ya kunyunyizia sukari. Endelea kukaanga hadi viive vizuri kisha miminia majani ya vitunguu yaliyokatwa katwa. Hakikisha yanachanganyika vizuri na wali wako kabla ya kuumimina kwenye sahani.
Pamba wali wako kwa viungo vilivyo pembeni. Kwanza chukua ndimu na kata kipande kisha weka kwenye sahani ya wali. Kisha chukua tango na katakata kwa mtindo utakaopendelea ili kuleta nakshi katika chakula chako. Tengeneza sosi ya kulia chakula chako kwa kuchanganya sosi ya samaki, pilipili na limao.
Ukitaka kula hakikisha unatumia sosi hii , kama mchuzi wake ili kuongeza ladha zaidi katika wali wako.
Chakula hiki kinaweza kuliwa mchana au hata usiku na kumfanya mlaji afurahie ladha yake.

Comments

Popular posts from this blog

Upishi wa tembele la chukuchuku

Tambi za nyanya

Tambi za dengu