Tambi za Nazi na vanilla

Mahitaji
Tambi 1/2kg
Chumvi kiasi Sukari kiasi
Tui bubu la Nazi, nusu kikombe cha chai
Vanilla
 Maji Lita moja

Namna ya kutengeneza

 
Chukua maji Lita moja na injika jikoni weka na chumvi kiasi. Acha yachemke na kisha vunja tambi zako na tosa kwenye maji hayo. Acha zichemke hadi zianze kuiva. Chuja maji kwenye tambi hizo na kisha mimina like tui bubu. Kisha weka sukari na baadaye matone matatu ya vannila. Acha zichemke ili maji yakakamie. Pakua kwenye sahani tayari kwa kuliwa. Katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani unaweza kula kama futari.

Comments

Popular posts from this blog

Upishi wa tembele la chukuchuku

Tambi za nyanya

Tambi za dengu