Dagaa kamba wa kukaanga


Mahitaji

Dagaa kamba ½ kilo
Unga wa dengu ¼ kilo
Chumvi
Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa kijiko 1
Mafuta ya kula ½ lita
Ndimu na pilipili kama unatumia
Masala .
Namna ya kufanya
Chukua dagaa kamba wasafishe wakate vichwa na uwamenye maganda yao na kuwaacha nyama ya ndani .
Waweke katika bakuli na kisha changaya na na viungo vyote tangawizi ,vitunguu saumu ,masala ndimu na pilipili chumvi.
Nyunyizia unga wa dengu katika mchanganyiko huo hadi upate uji mzito .

Chukua karai mimina mafuta weka jikoni na baada ya kuchemka kaanga dagaa wako hadi wawe na rangi chungwa .
Fanya hivyo kwa dagaa wote katika bakuli lako na baada ya hapo kamba wako wapo tayari kwa kuliwa waweza kula wenyewe kama kitafunwa au waweza kula kama kitoweo kwa kula na chakula kingine .

Comments

  1. Hongera Sana nahitaji hao dagaa ksmba walio kaanfwa tayari naweza kupata?

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Upishi wa tembele la chukuchuku

Tambi za nyanya

Tambi za dengu