Mkate wa mayai na jam
Mahitaji
Boflo kubwa 1
Mayai 4
Samli 1/4kg
Unga wa ngano kiasi
Namna ya kutengeneza
Kata mkate vipande vyembamba uvipake jam, kisha vigandishe kimoja juu kingine
Vunja mayai yapige sana. Kisha nyunyiza unga huku ukiendelea kupiga mayai
Injika chuma cha chapatti ( frying pan) utie samli ikianza kuchemka, chovya mikate iliyogandishwa katika mchanganyiko wa mayai na ngano na ukaange ndani ya chuma, ikiwiva geuza upande wa pili
Ikiwiva yaani ikiwa na rangi ya kahawia, vitoe na uvitie kwenye sahani. Tayari kwa kuliwa.
Huu ni mlo kwa ajili ya watu watatu
Comments
Post a Comment