Pudding ya mkate na siagi


Mahitaji
Mkate vipande vyembamba 2 au 3
Siagi 2 au3 vijiko vikubwa
Zabibu 1kijiko kikubwa
Maziwa 1kikombe
Yai 1
Vanila kijiko kidogo kimoja
Sukari 3 vijiko vikubwa

Namna ya kutengeneza

Paka siagi ndani ya bakuli.
chukua vipande vyako viwili vya mkate, paka siagi tia zabibu katikati ya vipande hivyo kisha vibane pamoja.
Weka ndani ya bakuli lako la bati
Koroga yai na kulichanganya vizuri pamoja na maziwa, vanila na sukari.
Mimina juu ya mkate katika bakuli .
Oka polepole katika jiko na kupakua ungali umoto.

Pudding yako ipo tayari kwa kuliwa, waweza kula na kinywaji chochote cha baridi.

Comments

Popular posts from this blog

Upishi wa tembele la chukuchuku

Tambi za nyanya

Tambi za dengu